Saturday, January 19, 2013

Ni kwa jinsi gani msomi anavyoweza kuleta mabadiliko chanya na pia kuleta hasara au kuwa chanzo cha matatizo ndani ya Jamii.


 Ni kwa jinsi gani msomi anavyoweza kuleta mabadiliko chanya na pia kuleta hasara au kuwa chanzo cha matatizo ndani ya Jamii.

Msomi ni mtu mwenye elimu ya jambo fulani. Katika nchi za kiafrika, kiwango cha elimu kimekuwa si cha kuridhisha ukilinganisha na nchi  zilizoendelea. Hali hii imezifanya serikali za nchi mbalimbali za kiafrika kutilia mkazo katika suala la elimu kwani elimu ni kiungo muhimu katika kufikia malengo ya maendeleo katika nchi yoyote duniani. Uchambuzi wa mada hii, unaegemea zaidi katika nchi zinazoendelea hasa za kiafrika na Tanzania ikiwemo.

Msomi anafaida kubwa na nafasi ya kuleta mabadiliko chanya ndani ya jamii. Umuhimu wa msomi ndani ya jamii ni pamoja na kufanya kazi mbalimbali za kitaalamu kama vile; udaktari, ualimu, uhandisi nk. Ufanyaji wa kazi hizi unapelekea kupata maendeleo na pia jamii kwenda sambamba na mabadiliko ya sayansi na technolojia.

 
Copyright © 2013. Mapalala Media