Ni kwa jinsi gani msomi anavyoweza kuleta mabadiliko chanya na pia
kuleta hasara au kuwa chanzo cha matatizo ndani ya Jamii.
Msomi ni mtu mwenye elimu ya jambo fulani. Katika nchi za
kiafrika, kiwango cha elimu kimekuwa si cha kuridhisha ukilinganisha na nchi zilizoendelea. Hali hii imezifanya serikali
za nchi mbalimbali za kiafrika kutilia mkazo katika suala la elimu kwani elimu
ni kiungo muhimu katika kufikia malengo ya maendeleo katika nchi yoyote duniani. Uchambuzi wa
mada hii, unaegemea zaidi katika nchi zinazoendelea hasa za kiafrika na Tanzania
ikiwemo.
Msomi anafaida kubwa na nafasi ya kuleta mabadiliko chanya ndani
ya jamii. Umuhimu wa msomi ndani ya jamii ni pamoja na kufanya kazi mbalimbali
za kitaalamu kama vile; udaktari, ualimu, uhandisi nk. Ufanyaji wa kazi hizi
unapelekea kupata maendeleo na pia jamii kwenda sambamba na mabadiliko ya
sayansi na technolojia.